Thursday, September 20, 2012

Niko Ambaye Niko Studio





New Gospel Studio in Tanzania
Location:    Mwananyamala, Dar es Salaam, Tanzania
Owner:        Steve Timothy Wambura
Producer:   Mr Zakayo from Dodoma

Activities:
  • Gospel Beats Production
  • Audio Recording (Choir, Solo Artists, Band)
  • Audio Advertisement (Radio Advertisement)
  • Live recording (Crusades, Sermons, Seminars, Choir live Performance)
  • Radio Programs
  • CD's Duplication
  • Music training ( Instruments, Singing and Performance)


Niko ambaye Niko Studio Inauguration day 
Bishop Lawrence Kameta (Left) making studio test, Steve Wambura (center) Bishop Swai (Right) In the studio during Inauguration day,

Rev Timothy Wambura in deep Prayers
TAG Deputy General Secretary Rev Timothy Wambura (Left) Praying for Niko Ambaye Niko Studio

Niko ambaye Niko Studio
With alot of Music Instrument

Rev Paul Mlokozi during inauguration of Niko ambaye Niko Studio

Many Pastors Attended the Opening Day


Wednesday, August 8, 2012

LOVE TANZANIA FESTIVAL WITH ANDREW PALAU

Love Tanzania Festival is a part of a larger story in Africa that involves 10 Capital Cities in 10 yrs.  A vision of International evangelist Andrew Palau - supported and invited by leaders in Africa.  Significant Festivals have taken place in Cairo, Egypt; Kigali, Rwanda; Kampala, Uganda; Bujumbura, Burundi and now on August 11-12 in Dar es Salaam.
800 plus churches will host Love Tanzania Festival with Andrew Palau. The Festival will take place at Jangwani Grounds and will feature:
  • a high energy Children’s program with DUGGIE DUG DUG from London, England;
  • Action Sports Demos (including FMX stunt team JUNGLE RUSH from Johannesburg, SA and BMX shows performed by ACTION SPORTS OUTREACH from San Diego, CA);
  • Food Vendors will be providing food each day so bring a little cash to buy something to eat. 
  • The Festival will also feature a world class Gospel Music show. 
  • The Main Stage will present local Tanzanian artists; THE VOICE, CHRISTINA SHUSHO, JOHN LISU plus a team of well-known worship leaders.
  • Tanzania’s much loved MASANJA will share his story, and
  • Dar es Salaam will also be blessed to host international Gospel Music sensations DON MOEN and NICOLE C MULLEN and DAVE LUBBEN.
  • Each day Andrew Palau will be with us to share a message of love and hope for Tanzania.  This event is a partnership between the Luis Palau Association based in Portland, OR in the USA and currently over 800 churches in the city. The local leadership planning this Festival involves nearly 200 people from every major denomination in the city. 

            ” This is a unique moment to celebrate, to come together to Love Tanzania.  Don’t miss it!”
                        Archbishop Valentino Mokiwa (One of the organizing Bishops)

Sunday, August 5, 2012

SARAH SHILLA FIRST GOSPEL ALBUM LAUNCH

Sarah Shilla first album Launch
NEW GOSPEL CEREBRITY IN TANZANIA
Name : Sara Shillah
Album: Let it rain In his Presence
Launching date: August 05, 2012
Venue: Banora hall, near Mlimani city business center

Sarah Shilla is a talented Tanzanian girl in gospel Music, she has been in music for quite long time, she has ministered in various palaces, including some churches in India and many churches in Tanzania, when in Tanzania she has invested her time in RIVERS OF JOY PRAISE TEAM of Tanzania Assemblies of God Victory Christian Center
Her father Rev Charles Shilla is a District General secretary of Tanzania Assemblies of God in Eastern region. and a senior pastor of TAG Makongo. so she has born in ministers family.

Her album launch was cerebrated by many gospel teams and artists including
  • Mwenge praise team
  • Eunice Hihatwa
  • Miriam Lukindo
  • John Sharaam
  • The Voice
  • John Lisu
  • Rivers of Joy
  • King Chavala - Gospel comedian 


Sarah Shilla gospel album lauch
 The album was launched by Guest of Honor Rev. Dr Huruma Nkone, the National director of CASFETA, and the senior pastor of Victory Christian Center.

Monday, May 14, 2012

SOS MISSION CRUSADE DAR ES SALAAM TANZANIA: THE GREAT CRUSADE EVER HAPPENED


MKUTANO MKUBWA WA INJILI
WA SHEREHE ZA ISHARA NA MIUJIZA
 Hii huduma ya SOS MISSION Ni huduma ya kimataifa iliyolenga kuwafikia watu wote duniani chini ya  Rev Johannes Amritzer , Wamejitawanya duniani kimatawi kuifanya huduma kufanyika kirahisi zaidi, Mungu anawatumia sana, kwa ishara na miujiza, kwa wanafunzi na watu ambao walifanikiwa kuhudhuria Campus night ya 11.11.2011 iliyoandaliwa na Kanisa la Victory christian Center Dar ni mashahidi. Mungu anawatumia hawa watu isivyo kawaida. 
SASA WAMEKUJA DAR TENA.
NJOO UMUONE MUNGU ANAVYOWATUMIA WATU, NJOO  USHUHUDIE MWENYEWE
 Rev Johannes Amritzer
 
Mahali:     Viwanja vya Jangwani, Dar es Salaam, Tanzania
Tarehe:      13 Jumatano hadi 17 Jumapili Juni 2012
Muda;       Kila siku saa 9 Alasili Mpaka 12:30 Jioni
Mnenaji:   Muinjilisti wa Kimataifa, Jonnes Amritzer



SOS Festival Band
Bendi ya sherehe za Huduma ya SOS Toka Sweeden


Kwaya mbalimbali na Waimbaji Binafsi  



Watakuwapo: Kinondoni Revival, Temeke Revival, The Reapers, Upendo Nkone, Christina Shusho, Bon Mwaitege
Mawasiliano,: +255 714 503 638, +255 762 441 719, email signsandwonderfestival_dar@vcc.org.tz

Friday, March 30, 2012

Tabia na Mahusiano kwa Mkristo


SOMO: TABIA NA MAHUSIANO
Mafundisho
Na Mr.Gammariel Chiduo

TABIA 6 ZA LAZIMA KATIKA KUJENGA USHIRIKA AU MAHUSIANO MAZURI
NA MUNGU, MKE /MUME, JAMII AU WATU WOTE

UTANGULIZI
·       Mwanadamu sio kisiwa, lazima akutane na ashirikiane na watu wengine /au na Mungu
·       (Mwanzo 1:26) Mungu anajifunua kwetu katika ushirika “NA TUFANYE MTU…”
·       Kuumbwa kwetu ni katika kutimiza takwa la USHIRIKA.
·       Umeubwa kwa ajili ya wengine
  •  Mungu amekuumba hivyo ulivyo kwa ajili ya wengine 
  • Ndio maana tuko tofauti sana. Mungu hajacopy na kupaste.  
  • Tofauti zetu huleta hitaji la USHIRIKA na kushirikiana
  • Utajikuta chochote unachofanya ni kwa ajili ya watu wengine. Mfano:
-         Unavaa kwa ajili ya watu, ili watu watakapokuona waone umependeza. Kioo kitakusaidia. Kama ni kwaajili yako vaa suti, ukalale au kaa chumbani.
-         Uhai wako ni kwa ajili ya watu. Ukitaka kujinyonga utashtakiwa. Jaribu kuwaambia kuwa uhai ni wangu, sasa nataka kuutoa kama watakuelewa.
·       Utajikuta unalazimika kujenga ushirika na wengine maana unawahitaji, na wanakuhitaji sana, hivyo hivyo ulivyo wewe ni wa thamani sana!!
·       Umoja ni jambo muhimu sana katika maisha yetu ya wokovu (Yoh 17:20-24) Yesu anatuombea tuwe na umoja.
·       Umoja ni kati ya vitu vinavyopigwa vita sana na shetani – ndiko kuliko na siri ya nguvu na ushindi.
·       (Mithali 30:27) Nzige hawana mfalme, lakini huenda makundi makundi.
·       Biblia inasema “ Mmoja hufukuza elfu, wawili makumi elfu!”
·       Wakutanikapo wawili au watatu mimi nipo hapo katikati yao.
·       Ukiwa na tabia 6 utajenga mahusiano mazuri
·       Tabia hizi ni kama CEMENT za kuunganisha matofali ili kujenga nyumba
·       Zikikosekana ni sawa na kupanga matofali bila cement.
·       Ziko tabia 6 za lazima zinazotumika kote kote, kwenye ushirika na Mungu, Mke au Mume na hata kwa watu wote:-

1.  Tabia ya UADILIFU na UTAKATIFU
·       Ili kujenga ushirika na uhusiano mzuri UADILIFU na UTAKATIFU ni tabia za lazima.
·       Kwenda sambamba na mnayowaza na kusema kwa pamoja.
·       Kama kuna ahadi inabidi kutimiza ahadi
·       Kutawafanya kuaminiana na kuimarisha umoja na uhusiano wenu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
(1Petro 1:15) Bali kama aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote.
v Utakatifu ndio tulioitiwa.
v Dhambi ndiyo iliyotutenga na Mungu
v Kutakaswa na kudumu katika utakatifu kutadumisha uhusiano wetu na Mungu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE/MUME
>> Uadilifu hujenga na kukuza mahusiano
>> Uovu na kusalitiana kwenye ndoa hata kama ni kwa siri, huvunja na kuua ushirika wenu. Ni kubomoa nyumba yenu kwa mikono yenu wenyewe. Mmejiloga wenyewe. Msitafute mchawi.



KWENYE UHUSIANO WAKO NA JAMII/WATU WOTE
v Watu hupenda mtu mwadilifu
v Humwamini mtu wa jinsi hiyo kwa kila kitu.


2. Tabia ya UKWELI na UWAZI
·       Tabia ya kuficha ukweli na uongo vinavunja Ushirika na urafiki.
·       Weka vitu vyote kwenye karatasi nyeupe mbele za watu wavielewe wavione.
·       Kama mmoja ana vitu asivyopenda kwa mwingine mawasiliano lazima yafanyike tena kwa heshima na taratibu ili kulinda umoja, kuliko kuweka moyoni

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
>> Ukweli utampendeza Mungu
>> Kuwa wazi mbele za Mungu kutaongeza kupendwa na Mungu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE/MUME
>> Mume au mke huchukizwa sana na vitu vinavyotendeka chini chini visivyoeleweka.
>>Mfano: Jamaa mmoja alimsave mpenzi wa nje kwenye simu yake kama Battery Low! Na mlio akauchagulia. Kila ikiita mke wake akiona Battery Low anaizima na kuiweka kwenye chaji. Uongo wa jinsi hii huharibu mahusiano kabisa, huna utakalojitetea mke au mume akakuamini tena.
>> Ukiwa mkweli na muwazi kwa mwezi wako utadumisha uhusiano wenu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA JAMII/WATU WOTE
>> Mtu mkweli na muwazi hupendwa na watu wote.

3. Tabia ya KUBADILIKA
·       Ukikubali kuwa hujakamilika, kwenye ushirika jipange KUBADILIKA
·       Kama kuna kitu hakijaenda vizuri angalia kama inakupasa UBADILIKE.
·       Badala ya kulaumiana jifunze kukubali KUBADILIKA.
·       Tabia ya kubadilika hukuweka uende sawa na sambamba na kukubalika.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
v Mungu anatarajia mabadiliko makubwa unapoendelea kumjua.
v Maana ya kukua kiroho ni kuongezeka na kubadilika kuelekea ukamilifu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE/MUME
>> Badilika unapogundua umekosea.
>> Badilika unapogundua mwenzako habadiliki.
>>Tumelelewa kwenye mazingira tofauti. Mila tofauti. Desturi tofauti.
>>Lipo jambo ambalo likitendeka kwa mwingine ni furaha, na kwa mwingine ni kero. Mfano: Kubanja. Ukiona kunamkera mwenzako BADILIKA anza kuona si tendo zuri.
>> Kubadilika kutawafanya mzidi kufanana na kuongeza utulivu kwenye ndoa.
>>Badilika unapoona misimamo yako haijengi.
(Epuka misimamo mikali, mimi nimeshasema basi… Siongei tena…n.k.)

KWENYE UHUSIANO WAKO NA JAMII/WATU WOTE
>> Mungu anatarajia mabadiliko makubwa unapoendelea kumjua.
>> Maana ya kukua kiroho ni kuongezeka na kubadilika kuelekea ukamilifu.

4. Tabia ya KUSAMEHE NA KUTUBU
·       Kukiri kosa na kuomba msamaha kunawashinda wengi
·       Au kusamehe baada ya kuomba msamaha ni kazi ngumu kwa wengi
·       Tabia ya kusamehe na kutubu ili usamehewe hujenga mahusiano kwa upya
·       Ukijizoeza kutubu kutakufanya urekebishe makosa uliyofanya
·       Kutubu na kusamehe kunahitaji unyenyekevu wa hali ya juu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
>> Kutubu hurejesha uhusiano wako na Mungu kwa upya.
>>Kuwasamehe wengine huimarisha uhusiano wako na Mungu na kuondoa kila kunyanzi moyoni.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE/MUME
>> Kosa linapotendeka, msamaha huhitajika kutoka pande zote mbili.
>>Kutokukiri makosa huharibu uhusiano kati ya mke na mume
>>Hata kama huoni kosa, na mwenzako analiona ni vema kuomba msamaha ili kurejesha uhusiano mzuri uliokuwepo, unaweza kugundua baadaye kuwa ulikuwa unakosea.  
>>Makosa yasiwe sababu ya kuwafarakanisha na kuharibu uhusiano wenu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA JAMII/WATU WOTE
>> Tabia ya kusamehe na kuomba msamaha kwa watu wote ni ya msingi katika kujenga mahusiano mazuri na watu.
>> Kutubu na kusamehe kunasaidia kuliweka wazi kosa na kuanzisha jitihada za kutolirudia badala ya kujenga ukuta wa kujilinda kwamba hujakosea, ni bahati mbaya


5.  Tabia ya HESHIMA na NIDHAMU
·       Ukitaka kuvunja kabisa uhusiano na mtu, onyesha unamdharau
·       Kila mtu anapenda kuheshimiwa
·       Dharau huharibu na kuvunja kabisa umoja na ushirika

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
>> Mungu anapenda kuheshimiwa
>>Mungu atazidi kukupenda unapoonyesha nidhamu na heshima kwake

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE/MUME
(1Petro 3:7) Mpe mke heshima…kusudi kuomba kwenu kusizuiliwe.
>> Heshima si kwa mume peke yake. Tunza heshima ya mke pia.
>>Kuheshimiana kunajenga umoja na mahusiano.
>>Tabia hii ya kuheshimiana hulinda na kuimarisha uhusiano wenu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA JAMII/WATU WOTE
>>Ukiwaheshimu watu wote wakubwa kwa wadogo, utajijengea uhusiano mzuri na watu wote.

6. Tabia ya KUTOA /KUJITOA
·       Tatizo kubwa la msingi au SUMU  ya ushirika ni UBINAFSI.
·       Ubinafsi ni uchawi unaologa na kuusambaratisha umoja na ushirikiano
·       Kwenye mahusiano au ushirika usisubiri wewe tu upewe, tafuta nafasi ya kutoa

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MUNGU
>>Yeye alimtoa Kristo.
>>Mungu ametupa vyote tulivyonavyo, sisi ni mawakili tu.
>>Unatazamiwa ujitoe zaidi na umtolee zaidi kuonyesha kiasi gani unampenda.



(Mwanzo 22:15-18) IBRAHIM AKIMTOA ISAKA
Ibrahimu anamtoa Isaka, yuko tayari kumchinja Mungu akasema “Nimeapa kwa nafsi yangu, kwa kuwa umetenda neno hili; wala hukunizuilia mwanao, mwanao wa pekee, 17katika kukubariki nitakubariki, na kama mchanga ulioko pwani; na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao, 18na katika uzao wako mataifa yote ya dunia watajibarikia; kwa sababu umetii sauti yangu.

KWENYE UHUSIANO WAKO NA MKE /MUME
(             )  Msinyimane
>>Wote wawili uhusiano utadumu na kuongezeka zaidi kama kila upande unazingatia kutoa.
>> Zawadi ndogo ndogo na kubwa kutoka kila upande husherehesha uhusiano wenu.

KWENYE JAMII NA WATU WOTE
Utapendwa na watu, utajipatia marafiki wengi ukiwa mtoaji
(Mhubiri ) Mali ikiongezeka, walao nao huongezeka
(Luka      ) Wapeni watu vitu, nanyi mtapewa kwa kipimo cha kujaa na kusukwa sukwa


SUMMARY
TABIA 6 ZA LAZIMA KATIKA KUJENGA USHIRIKA
1.    TABIA YA UADILIFU NA UTAKATIFU
2.    TABIA YA UKWELI NA UWAZI
3.    TABIA YA KUBADILIKA
4.    TABIA YA KUSAMEHE NA KUTUBU
5.    TABIA YA HESHIMA NA NIDHAMU
6.    TABIA YA KUTOA NA KUJITOA

Tabia hizi hata kama unazo, ongeza viwango vyake, utajenga ushirika na mahusiano mazuri.

Mr Gamariel Chiduo
TAG Head Office